
Majambazi 13 kati ya 17 wanaowahangaisha wenyeji huko mlima Elgon kaunti ya Bungoma wamekamatwa. Waziri wa usalama Dr.Fred Matiang’ anasema polisi wanaondeleza misako zaidi kuwanasa majambazi wengine kuhakikisha usalama eneo hilo. Akiwahutubia wakuu wa polisi hapa Nairobi, Dr.Matiang’ amewataka wakenya hasa maeneo ya Bonde la Ufa na Kaskazini Mashariki kushirikiana na polisi kuhakikisha taifa linasalia salama.