Swahili Videos
Huduma za treni zalemewa na idadi kubwa ya wasafiri hasa Nairobi

Waziri wa uchukuzi James Macharia amesisitiza ya kwamba serikali itaendelea kutumia treni na njia nyinginezo kuwezesha wakenya ambao wameathirika kufuatia msako wa magari ya uchukuzi wa umma unaoendelea nchini.
Haya yanajiri huku wengi wa abiria kutoka sehemu mbalimbali jijini Nairobi wakikosa treni hizo leo asubuhi kutokana na idadi kubwa ya wasafiri.