HabariK24 TvSwahiliSwahili VideosTop StoriesVideos
Madawa aina ya Mandrax zaidi ya 800,000 yanaswa, Eldoret

Polisi kutoka kaunti ya Uasin Gishu wamewatia mbaroni maafisa wanne wakiwemo watatu kutoka halmashauri ya ushuru (KRA) na mmoja kutoka bodi ya kusimamia dawa nchini.
Maafisa hao walipatikana na dawa za kulevya aina ya Mandrax katika uwanja wa ndege wa Eldoret.
Baada ya kufanyiwa ukaguzi wa kimaabara dawa hizo zilibainika kuwa za Mandrax na sio za virutubisho kama ilivyodaiwa kwenye stakabadhi.