
Huduma za matibabu zimerejelea katika hospitali ya St. Marys Langata hapa Nairobi baada ya huduma hizo kusambaratika kufuatia mzozo wa usimamizi. Maurice Audi msimamizi mpya wa hospitali hiyo amewataka wagonjwa walioondoka hospitalini humo jana hasa katika kitengo cha watoto kurejea na kuendelea na matibabu. Amekana madai yaliyotolewa na waliokuwa wafanyikazi kuhusiana na huduma zinazotolewa.